Sunday, June 19, 2011

HAVING THE RIGHT ATTITUDE

Abdallah ni miongoni mwa watu wenye ujasiri na uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto za maisha. Ni jasiri kwa sababu ameweza kupambana na ulemavu wa macho alioupata ukubwani, na kuhakikisha anajitafutia maisha kwa njia halali. Yeye kwa sasa ni miongoni mwa mafundi hodari wanaokubalika ndani na nje ya nchini. Je, ilikuwaje hata akawa katika hali ya ulemavu aliyonayo sasa?