Saturday, November 5, 2011

Tano Tano Za Kujipanga Kwa Kazi!

Hatua 5 Za Kujipanga Kwenye Kutafuta Kazi

1. Malengo! Uwe na dira na malengo binafsi, ujue sifa na nguzu zako ili utafute fursa za kuzikuza, fanya utafiti wa mashirika yanayoweza kukufikisha mwenye malengo yako binafsi.

2. Jipange! Andaa wasifu na barua ya maombi ya kazi zinayokuwakilisha vizuri kwa maelezo na muonekano na mpe mtu apitie kutathmini ubora na usahihi wa maelezo na muonekano.

3. Usibahatishe! Tuma sehemu sahihi na kwa mtu sahihi. Tuma kwa mashirika unayoona yanaendana na malengo yako binafsi, tafuta kujua nafasi sahihi kwenye shirika na hata mtu husika atakayepokea maombi ili uandike jina lake kwenye hiyo barua.

4. Rahisisha! Tumia computer na kutuma barua ya maombi kupitia barua pepe (hii ni rahisi zaidi kuliko kutumia sanduku la posta) na uambatanishe wasifu.

5.  Ng'ang'ania! Fuatilia maombi ya kazi baada ya wiking'ang'ania!  kwa njia ya simu, barua pepe ama nenda mwenyewe. Heshimu jibu watakalokupa. Ukiambiwa watakujibu baada ya muda fulani na wiki ikapita baada ya huo muda, watafute tena.